Thursday, September 9, 2010

KWENU WADAU WANAOTAKA KUJIUNGA

CHAMA CHA WANYWAJI




Nimeanzisha chama changu,



Nani anataka kujiunga?????



Itabidi tujaze kwanza fomu za kugombea

urais, nimeshamuhonga msajili wa vyama na mwenyekiti

wa tume ya uchaguzi kwa hiyo ingawa tumechelewa

hatutapata shida.



kabla ya sera tunaanza na majukumu, hebu kwanza pata

undani.......................................





ZIFUATAZO NI ADHABU ZITOLEWAZO KWA UVUNJAJI WA SHERIA

ZA CHAMA CHA WANYWAJI



1. Kosa la kumtoroka mlevi mwenzako kwenye bar - Jela

miezi tisa



2. Kuacha kunywa pombe na fedha unazo - Kifungo cha

maisha



3. Kuvunja chupa ya beer - Jela miaka miwili



4. Kumkaribisha mume au mke wa rafiki yako bila idhini

yake - Viboko ishirini vya makalio na kufungiwa kunywa

nusu siku



5. Kuomba kununuliwa chakula au kununua chakula au

bidhaa kwa wamachinga wakati wa kukata maji, na ukijua

dhahiri pesa ya pombe inapungua - Jela miezi tisa



6. Kumchukulia dhamana mtu asiyepiga (mma) pombe

adhabu yake ni - kutolewa kwenye chama



7. Kumwibia pombe mlevi mwenzako ni kosa kubwa - Jela

mwaka mmoja



8. Kukataa kunywa wakati umekaribishwa - Jela miaka

mitano



9. Kukwepa ulevi wa aina yoyote adhabu - kunyang'anywa

mke au mume kama huna utaozwa/kuozeshwa mke au mume

kwa nguvu



10. Kupita Bar au Grocery na kujifanya huoni hilo ni

kosa kubwa faini yake ni -kuwanunulia wanywaji wote

waliokuwa kwenye Bar/Grocery kila mtu kinywaji

anachokunywa na kukaa ukiwaangalia hadi wamalize



11. Kumcheka mnywaji mwenzako akiwa amelewa ni kosa la

jinai, unachotakiwa kufanya ni kumpongeza kwa kazi

nzito aliyofanya, adhabu yake ni - Kutolewa kwenye Bar

muda wa dakika moja



12. Kumshawishi mlevi kuacha pombe kwa kisingizio eti

ajenge nyumba au asomeshe watoto - Kunyongewa Bar



13. Kukataa kunywa kwa madai unajenga adhabu ni -

kuwanunulia bia wenzako hadi utakapomaliza ujenzi



14. Ukinywa pombe halafu utapike adhabu ni - Kurudia

kunywa hadi ulewe tena



Wenu mshiriki

No comments:

Post a Comment